Top News

Mbunge Maganga aungana na Kamati ya Madiwani kufuatilia Mapato ya Halmashauri Migodini

 

MADIWANI WASHTUKIA UPIGAJI WA MAPATO YA SERIKALI.

NA ANTHONY SOLLO MBOGWE.

KUFUATIA kudorora kwa ukusanyaji wa Mapato ya  Halmashauri,Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita limeunda Kamati Maalumu ya ufuatiliaji wa Mapato ya Migodi iliyoko katika Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Kamati hiyo inaongozwa na Mwenyekiti Marco John Nzella huku wajumbe wa Kamati hiyo wakiwa ni pamoja na Lucy Samwel,Paul Edward Ngussa,pamoja na Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Nicodemus Maganga.

Kamati hiyo pia imeambatana na Wataalamu kutoka Serikalini ambapo miongoni mwa watumishi hao ni pamoja na Eng Yohana Marwa anayemwakilisha Ofisa Madini Mkazi Mkoa wa Kimadini wa Mbogwe,Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe pamoja na Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Nicodemus Henry Maganga akizungumza na wananchi katika Mgodi wa Isanjabadugu ulioko Nyakafuru.
Wananchi wakimpokea kwa shangwe Mbunge wao baada ya kuwasili katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Nyakafuru Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita.


Mbunge wa Jimbo la Mbogwe akisaini Kitabu cha wageni alipowasili katika Mgodi wa Kanegele Namba moja

Mbunge wa Jimbo la Mbogwe akiteta Jambo na Mkurugenzi wa Mgodi wa Kanegele Namba moja Bwana Elias Kisome baada ya kuwasili akiambatana na Kamati Maalumu iliyoundwa na Madiwani kwa lengo la kufuatilia Mapato ya Halmashauri hiyo.


Wakiwa katika Mgodi wa Kanegele Namba Moja Maarufu kwa mchungaji, Kamati hiyo imepokelewa na kufanya majadiliano kwa saa kadhaa huku ikiomba taarifa ya Mapato ya March 2024 ambapo Mkurugenzi wa Mgodi huo Elias Kisome alijitetea mbele ya Kamati hiyo,kuwa kutokana na ajali iliyotokea katika Mgodi huo shughuli za uzalishaji zilisimama.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Mgodi wa Kanegele Namba Moja Elias Kisome ameiambia Kamati hiyo kuwa baada ya kuanza kwa shughuli za uzalishaji Mgodi huo umelipa jumla ya Tshs Mil 8.kwa ajili ya maombi ya kupeleka mawe kwenye Mtambo wa kisasa unaotumika  kuchakata mawe yanayosadikiwa kuwa na Dhahabu (CIP)

Baada ya majadiliano na Kamati mjumbe wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Nicodemus Maganga alifanya mkutano na wachimbaji wanaofanya shughuli zao katika Mgodi huo huku akihamasisha wananchi kwenda kujiandikisha katika Vituo kwa ajili ya uboreshaji wa taarifa katika Daftari la Kudumu la Wapiga kura

Licha ya kuhamasisha wananchi kwenda kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga kura Mbunge Maganga alikaribisha wananchi kutoa maoni pamoja kero ambapo Solomon Mathayo alimuomba Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Nicodemus Maganga kutumia nafasi yake kama mwakilishi wa wananchi kuishawishi Serikali kufanya mabadiliko ya Sheria ya Madini.

"Nikuombe sana mheshimiwa Mbunge wetu uende kuitumia nafasi yako kama mwakilishi wa  wananchi kuishawishi Serikali kufanya mabadiliko ya Sheria ya Madini ili iweze kwenda na wakati maana sisi kama wachimbaji tunapata shida kubwa hasa tunapogundua Madini katika maeneo yetu.

Katika hatua nyingine akiendelea na ziara yake Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Nicodemus Maganga ameendelea na ufuatiliaji wa Mapato katika Mgodi wa Migodi katika maeneo ya Mwagimagi na kuhitimisha ziara yake katika Mgodi wa Nyakafuru na kisha kuzungumza na wananchi ambapo pia kilio Chao ni utitiri wa Tozo za Halmashauri










Post a Comment

Mpya zaidi Nzee zaidi