Madiwani matatani kwa
kukipaka Matope CCM.
Na Antony Sollo KAHAMA.
MADIWANI wa Kata ya
Nyahang
Akizungumza na Waandishi
wa Habari Askofu Mkuu wa Kanisa la Makimbilio Riziki Esromu alisema kuwa baada
ya kununua maeneo hayo akiwa anayaendeleza kila mwaka kwa kupanda miti na mazao
ya muda mfupi kama mpunga ndipo Madiwani hao wawili Panklas Ikongoli na yule wa
Viti Maalumu Helena Bundala walifika na kulazimisha kupatiwa viwanja vinne ili
wavimiliki.
Hata hivyo baada ya
ombi hilo kugonga mwamba wawakilishi hao wa wananchi kupitia Chama cha
Mapinduzi walimpa vitisho Askofu huyo kuwa kwa kuwa amegomea ombi lao
watakwenda kusimika bendera ya Chama cha Mapinduzi katika maeneo yake ili
anyang’anywe kwa kupitia mgongo wa Chama.
Askofu Mkuu wa Kanisa
la Makimbilio Riziki Esromu alinunua maeneo hayo mwaka 2011 kutoka kwa watu
tofauti tofauti katika eneo lililoko Mtaa wa Mtakuja amblo kabla ya mabadiliko
ya Kiutawala lilikuwa Kijiji cha Shunu Kitongoji cha Kagera.
Gazeti hili limeweza kupata Nakala za vielelezo vinavyothibitisha umiliki wa maeneo hayo kutoka kwa wananchi kwenda kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Makimbilio ambapo baada ya kutaka kujiridhisha Mwandishi wa Habari alimtafuta Diwani Helena Bundala ili kutolea ufafanuzi juu ya tuhuma hizo.
Akizungumza na gazeti
hili Diwani huyo aliruka futi elfu kumi na kudai kuwa hana taarifa za uwepo wa
Mgogoro katika eneo hilo.
“sina taarifa za kuwepo
kwa Mgogoro baina yangu na Askofu huyo na sijawahi kwenda kwake kuomba eneo
hivyo taarifa hii ni ngeni kwangu”alisema Bundala.
Hata hivyo gazeti hili
limeshuhudia baadhi ya jumbe fupi za simu za mkononi wakiwasiliana na Askofu
Mkuu wa Kanisa la Makimbilio kuhusiana na kutaka kupatiwa maeneo ambapo baada
ya kusikika kuwa suala hilo linafuatiliwa na waandishi wa Habari ameamua
kujiweka pembeni.
Katika mwendelezo wa
vitisho alivyopatiwa Askofu huyo ushahidi umeonyesha kuwa yale waliyoyasema ni
kweli Madiwani hao walimpandikiza mtu aliyejulikana kwa jina la Stephen Joseph
Kafumu ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti Mstaafu wa chama cha Mapinduzi Kata ya
Nyahanga kuwa mmiliki wa eneo hilo ambaye hata hivyo hana nyaraka yoyote
kuthibitisha umiliki wa eneo hilo.
Akizungumzia Sakata la
kutishiwa na Madiwani hao Askofu Mkuu wa Kanisa la Makimbilio Riziki Esromu
Makanika alisema kuwa akiwa katika Ofisi ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Mtakuja
Julius Sabuni Disemba 19 . 2022 baada ya mahojiano alipoulizwa kama ana nyaraka
yoyote inayoweza kuchukuliwa kama ushahidi kwa ajili ya kuthibitisha umiliki
wake wa eneo alisema hana bali eneo hilo ni la ukoo.
Gazeti hili lilimtafuta
Diwani wa Kata ya Nyahanga Panklasi Ikongoli ili kutolea ufafanuzi tuhuma za
kutoa vitisho kwa Askofu wa Kanisa la Makimbilio alisema kuwa hawezi kuzungumza
chochote kutokana na kwamba hayuko katika maeneo mazuri kuzungumza.
“sitaweza kuzungumza
chochote njoo Ofisini tuzungumze kwa nini usije?leo ni siku ya mapumziko leo
siwezi kuzungumza,ukipata nafasi njoo Ofisini”alisema Ikongoli.
DIWANI AFUNGA OFISI YA BARAZA LA KATA NYAHANGA.
Uchunguzi uliofanywa na
gazeti hili umebaini kuwa baada ya kukosekana kwa ushahidi kutoka kwa Stephen
Kafumu ambaye alitengenezwa na Diwani huyo kuwa ni mmiliki wa eneo hilo Diwani
Ikongoli aliamua kufunga Ofisi za baraza la Ardhi la Kata ili kupinga kutolewa
kwa Hati ya kushindwa kusuluhisha ili mlalamikaji asiende mbele.
“Ndugu mjumbe wa baraza
la Kata ya Nyahanga pokea taarifa kwamba baraza limesimamishwa rasmi kuanzia
leo tarehe Disemba 28 2022 hadi hapo mapema januari 2023 kikao cha WDC
kitakapokaa wasiliana na WEO kwa Utekelezaji”ilisema sehemu ya ujumbe huo ambao
ulisambazwa kwa wajumbe wa baraza hilo.
Gazeti hili lilimtafuta
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Nyahanga Lucas Matanyanga ili kutolea ufafanuzi
kuhusiana na tuhuma dhidi ya Madiwani hao ambapo alikiri kupokea malalamiko na
kusema Ofisi yake inafanyia kazi na ikikamilisha na kubaini ukweli itachukua
hatua stahiki.
“Ni kweli Ofisi yangu
ya Chama cha Mapinduzi imepokea
malalamiko kuhusu Mgogoro huo,Ofisi yangu inafanyia kazi na ikikamilisha na
kubaini ukweli tutachukua hatua stahiki”alisema Matanyanga.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kahama Thomas Muyonga ili
kuzungumzia Sakata la Madiwani wa Kata ya Nyahanga kutoa Vitisho kwa Askofu
Mkuu wa Kanisa la Makimbilio Riziki Esromu Makanika ambapo alisema hana taarifa
juu ya malamiko hayo lakini akasema Chama cha Mapinduzi hakina utaratibu wa
kupora maeneo ya watu badala yake kinatetea wananchi kwa maslahi mapana ya
kulinda Amani na Utulivu kwenye jamii.
Kuhusu suala la
Madiwani hao kuanzisha mgogoro baina ya watumishi wa Mungu kwa kivuli cha chama
Mwenyekiti huyo alisema iwapo itabainika kuwepo kwa matumizi mabaya ya jina la
Chama chama hakitasita kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya Madiwani hao.
“Chama cha Mapinduzi hakina utaratibu wa kupora maeneo ya watu badala yake kinatetea wananchi kwa maslahi mapana ya kulinda Amani na Utulivu kwenye jamii,kuhusu suala la Madiwani hao kuanzisha mgogoro baina ya watumishi wa Mungu kwa kivuli cha chama Mwenyekiti huyo alisema iwapo itabainika kuwepo kwa matumizi mabaya ya jina la Chama chama cha Mapinduzi hakitasita kuchukua hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni za Chama dhidi ya Madiwani hao”alisema Mwenyekiti wa CCM Kahama.
Pichani ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Mlima wa Makimbilio (HMM) Riziki Esromu Makanika akionyesha mawe yaliyowekwa na baadhi ya watu waliouziwa viwanja na Madiwani wa Kata ya Nyahanga ambao wanadaiwa kumtishia Askofu huyo Picha na Antony Sollo.

Chapisha Maoni