Top News


Mfumo wa Stakabadhi ghalani kuondoa changamoto ya wakulima kukopwa Mazao yao.

Na Antony Sollo DODOMA.

 MKURUGENZI wa Bodi ya usimamizi wa Stakabadhi ghalani Asangye Bangu amesema Mfumo wa Stakabadhi za Ghala utaondoa changamoto ya wakulima kukopwa mazao yao na wafanyabiashara.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Jijini Dodoma Bangu alisema kuwa dhumuni la Kuanzishwa kwa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ni kukuza juhudi za Serikali,kurasimisha mifumo ya masoko iliyopo kwa lengo la kupunguza vipingamizi mbalimbali vinavyokwaza uzalishaji wenye tija na utafutaji masoko kwa bidhaa mbalimbali hususan mazao ya kilimo

 Bangu alisema,mfumo huo unawawezesha wazalishaji bidhaa kukusanya na kuweka katika Ghala Kuu kwa malengo ya mbalimbali ikiwemo kuuza kwa pamoja kupitia minada ya pamoja kwa lengo la kupata bei nzuri kupata huduma za kifedha kama vile mikopo na kuhifadhi ghalani ili kurahisisha usindikaji.

 Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Bodi ya usimamizi wa Stakabadhi ghalani Asangye Bangu Stakabadhi ya Ghala ni hati Maalumu inayotolewa kwa Meneja Ghala/Meneja Dhamana kwa mweka mali katika Ghala Kuu inayotaja umiliki, idadi na sifa za ubora wa mali iliyowekwa ghalani kwa mujibu wa Sheria hati hii huchapwa na kutolewa na Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala pekee.

Mkurugenzi huyo alieleza kuwa,Mfumo huu una manufaa makubwa ikiwemo kuwapa nguvu waweka mali hususani wakulima kupigania bei nzuri katika soko kwa kuhamasisha kutumia mfumo wa pamoja kukusanya na kuuza, kutoa uhakika wa ubora na bidhaa na Mfumo wa uthibitisho na kupunguza mashaka na gharama za ushughulikiaji.

Hurahisisha pia kuondoa mashaka kwa wafanyabiashara wa bidhaa na wakulima wakati wa kufanya biashara kuweka utaratibu wa kupata taarifa takwimu za soko na mauzo,taarifa za kuaminika kwa wadau mbalimbali kuongeza ushiriki wa wafanyabiashara wa bidhaa wenyeji katika biashara ya kimataifa,kuhimiza usindikaji wa mazao ya msingi kwa lengo la kuongeza thamani na kukuza uendelezaji wa viwanda.

kuongeza upatikanaji wa sehemu za kuhifadhia mazao zilizo bora, kupunguza hasara za baada ya kuvuna na kuimarisha uhakika wa upatikanaji wa chakula na kuongeza wigo wa wananchi kuweza kukopa katika asasi za fedha kwa kutumia mazao yao kama dhamana.

Akizungumzia Utekelezaji wa mfumo huo nchini Tanzania Bangu alisema kuwa Kufuatia vikwazo mbalimbali katika mauzo ya bidhaa za wazalishaji wadogo hususan mazao ya kilimo nchini mwaka 1999 Serikali iliendesha mradi utafiti wa mbinu bora ya kuwawezesha wakulima kupata bei nzuri katika mazao kupitia ukusanyaji wa pamoja na kuuza kwa njia ya Stakabadhi ya Ghala.

Baada ya kufanikiwa kwa majaribio hayo, mwaka 2005 Sheria ya Stakabadhi za Ghala ilipitishwa na Bunge na kuanza kutumika katika msimu wa mwaka 2007/8 katika zao la korosho.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa tangu kuanza kutumika kwa Sheria ya Stakabadhi za Ghala, mfumo umetekelezwa katika mazao 11 yaliyoleta makusanyo zaidi ya kilogramu bilioni 2.3 hadi kufikia Robo ya Kwanza ya Mwaka 2021/22.

Kuhusu Mafanikio Bangu alisema kuwa,katika Mazao mbalimbali mafanikio yaliyopatikana baada ya kuanzishwa kwa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ni pamoja na (i) ongezeko bei la bei za mazao, mapato ya mkulima na mapato ya Serikali kwa wastani wa asilimia 200% kutokana na urasimishaji.

Mafanikio mengine ni pamoja na ongezeko la uzalishaji wa mazao kwa wastani wa asilimia 12% kwa mwaka,kichocheo cha ubora wa mazao yanayofikishwa sokoni,upatikanaji wa takwimu sahihi za mazao yanayopita kwenye Mfumo wa Stakabadhi za Ghala,ongezeko la mapato ya uhakika kwa Serikali Kuu na Serikali Mitaa,kukuza huduma za fedha vijijini ili kufanikisha uanzishaji wa Soko la Bidhaa Tanzania.

 Kuhusu zao la Korosho Mkurugenzi huyo alisema kuwa baada ya kuanzishwa kwa Mfumo, mwenendo wa bei na ushalishaji ulibadilika ghafla na kuanza kuwa na mwenendo chanya positive trend ambapo mara baada ya kuanzishwa kwa Mfumo palikuwa na ongezeko la asilimia 164% la bei kutoka Ths 350.00 msimu wa 2006/07 hadi kufikia Tsh 925.00 msimu wa 2007/08.

Hata hivyo Bangu alisema tangu kuanza kwa Mfumo katika miaka minane ulipoanzishwa Mfumo huu kwa maana ya 2007/08 hadi 2014/15 wastani wa ongezeko la bei kwa mwaka ulikuwa 25% kulinganisha na ongezeko la bei miaka minane kabla ya kuanzishwa kwa Mfumo ambapo ilikuwa ni asilimia 12% kwa mwaka kaunzia mwaka 1998/99 hadi 2006/07.

Post a Comment

Mpya zaidi Nzee zaidi