Top News

 

 

Tatizo Uhaba wa Mafuta lawaibua wabunge.

NA  ANTHONY SOLLO - DODOMA. 05.Sept 2023

WAKATI Vikao vya Bunge vikiendelea Jijini Dodoma Wabunge wameishauri Serikali kutafuta namna bora ya kukabiliana na changamoto ya uhaba wa Mafuta inayoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.

Wakizungumza na waandishi wa Habari katika viunga vya Bunge Jijini Dodoma Wabunge hao wamekiri kuwepo kwa uhaba wa mafuta katika maeneo mbalimbali nchini n ahata katika majimbo yao.

Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro Emmanuel Oleshangay alisema hali ya ukosefu wa mafuta inaathiri uchumi wa wananchi pamoja na Taifa kwa ujumla wake na kuongeza kuwa katika Jimbo hilo ni vituo viwili tu vya mafuta vinavyotoa huduma hiyo  lakini kwa muda wa takribani wiki mbili sasa hawapati mafuta ya Petrol na hata Dizeli.

Aidha Mbunge huyo wa Jimbo la Ngorongoro Emmanuel Oleshangay alisema kuwa kazi ya wabunge ni kuisimamia na kuishauri Serikali,hasa katika masuala ya maendeleo ya nchi pamoja na yale ambayo yanawaumiza wananchi hata hivyo Mbunge huyo aliishauri Serikali kutafuta muarobaini ili kuona namna namna nzuri ya kuagiza mafuta kupitia (BPA) Bulc Procurement Argency na pia aliishauri Serikali iweke akiba ya mafuta yatakayokuwepo angalau kwa kipindi cha miezi sita ili kukabiliana na tatizohilo.

“Ni kweli kuna uhaba mkubwa wa mafuta ya Petroli na hata Dizeli,na mara kadhaa kama Wabunge tulishalitolea taarifa jambo hili kwa kuishauri Serikali iweke akiba ya mafuta angalau kwa kipindi cha miezi sita hivyo tunaendelea kuishauri itafute namna bora ya kukabiliana na tatizo hili”alisema Oleshangay.


Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro Emmanuel Oleshangay Picha na Maktaba.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Costantine John Kanyasu ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini alipotakiwa kutolea ufafanuzi kuhusu uhaba wa mafuta maeneo mbalimbali nchini likiwemo Jimbo la Geita Mjini Mbunge huyo pia alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo.

Tatizo hili la uhaba wa mafuta linalotokea mwezi huu wa tisa kama wabunge tulilijua tangu mwezi wa saba kutokana na trend ya uingizaji wa mafuta lakini pia na trend ya uhaba wa fedha za kigeni (USD)

“sisi kama Wabunge jambo hili linatusikitisha sana kwa sababu linaathiri mfumo mzima wa uchumi wa wananchi wet una kusababisha kupanda kwa gharama za Maisha “alisema Kanyasu.

Kanyasu amesema,kutokana na uhaba wa mafuta wananchi wanapokosa mafuta katika vituo vya mafuta vilivyosajiliwa kihalali wanalazimika kwenda kununua mafuta hayo kwa walanguzi badala ya Sh 3400/3500 wananunua kwa gharama kati ya Sh 4500 hadi 5000.

Kwa hiyo hili ni jambo kubwa linaathiri uchumi katika Nyanja zote ikiwemo usafiri,gharama za bidhaa na Maisha yanapanda,kanyasu alisema,jambo la msingi ni kwamba tatizo hili ni la kidunia (Global) ambalo linaanza na kuyumba kwa Uchumi wa Dunia lakini pia ni pamoja na vita vinavyoendelea.

Mbunge huyo ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini alisema Kamati hiyo imeishauri Serikali kutafuta kila aina ya mbinu za kukabiliana na tatizo hili ikiwemo kutafuta msaada kwa nchi marafiki ,Akiba zilizopo katika nchi na kutumia bidha zilizopo nchini ili kuweza kulimaliza tatizo hili.

“Mfano mpaka sasa tunavyoongea mafuta yabo Bandarini lakini hayawezi kushushwa kwa sababu mwenye meli anataka alipwe fedha zake kwanza na kinachopelekea kutoshushwa kwa mafuta hayo ni kutokana na uhaba wa dola”alisema Kanyasu.

Kuhusu Halmashauri zilizofikia hatua ya kutokopesheka kutokana na kudaiwa madeni na wauzaji wa mafuta,Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Costantine John Kanyasu alisema kuwa,Halmashauri ya Mji wa Geita ina viongozi mahiri wakiwemo Madiwani wa Halmashauri hiyo ambao wanatekeleza vizuri majukumu yao kwa uaminifu mkubwa huku akimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Zahara Muhidin Michuzi kwa usimamizi mzuri matumizi ya fedha za Serikali.

 “Kuhusu madeni sisi katika Halmashauri yetu tuko vizuri,Halmashauri ya Mji wa Geita ina viongozi mahiri wakiwemo Madiwani wa Halmashauri ambao wanatekeleza vizuri majukumu yao tena kwa uaminifu mkubwa napenda mpongeza kwa dhati Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Zahara Muhidin Michuzi kwa usimamizi mzuri matumizi ya fedha za Serikali.

 

Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Costantine John Kanyasu Picha na Maktaba.

 


Post a Comment

Mpya zaidi Nzee zaidi