Top News

 

Miaka Mitatu ya Rais Samia,Uongozi wa Mgodi wa Mwagala Gold Mine wamwaga mamilioni kwa jamii.




Pichani ni picha za Mitambo mbalimbali inayotumika katika shughuli za uchimbaji na uchakataji wa Madini katika Mgodi wa MWAGALA GOLD MINING (MGM)ulioko katika Kijiji cha Igurubi Kata ya Igurubi Halmashauri ya Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora 

NA ANTHONY SOLLO  IGUNGA.

MENEJA wa Mgodi wa MWAGALA GOLD MINING (MGM)ulioko katika Kijiji cha Igurubi Kata ya Igurubi Halmashauri ya Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora Steven Emmanuel Siame,ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji nchini.

Akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu miaka mitatu ya Rais Samia Meneja wa Mgodi wa Mwagala Steven Emmanuel Siame amesema,katika kipindi hiki cha miaka mitatu ya Rais Samia,wachimbaji wadogo wamenufaika na namna Rais alivyofanikiwa kuifungua nchi hasa uwekezaji katika Sekta ya Madini hususani kwa wachimbaji wadogo na wakati.

“katika kipindi hiki cha miaka mitatu ya Rais Samia,sisi wachimbaji wadogo tumenufaika na namna Rais alivyofanikiwa kuifungua nchi hasa kwa kukaribisha uwekezaji katika Sekta ya Madini hususani kwa wachimbaji wadogo na wakati”anasema Siame.

Katika hatua nyingine Meneja wa Mgodi wa Mwagala Gold Mining Steven Siame ameipongeza Serikali kwa kufuta Leseni za Utafiti zinazochukua maeneo makubwa huku zikiwanyima wachimbaji wadogo fursa ya kuwekeza.

“Naipongeza Serikali kwa uamuzi wake wa kufuta Leseni za Utafiti zilizokuwa zinazochukua maeneo makubwa jambo ambalo lilipelekea kuwanyima wachimbaji wadogo fursa ya kuwekeza”anasema Siame.

Akizungumzia changamoto Meneja huyo pia ameiomba Serikali iwasaidie wachimbaji wadogo ikiwa ni pamoja na kuwaongoza namna ya kupata Msaada wa kufanya Utafiti wa miamba katika maeneo yao pamoja na kupata Mitaji yenye tija.

Ameiomba Serikali kupitia GST mbaye ni mlezi mama kwa wachimbaji wadogo na wa Kati kuwapata fedha kwa wakati ikiwemo Mikopo yenye masharti nafuu kutoka Taasisi za Fedha na kutoa wito kwa wawekezaji kutoka nje kujitokeza kwa wingi ili kuungana na kuweka mazingira mazuri ya Kiufundi na Teknolojia itakayoweza kuongeza Mapato ya Kampuni pamoja na Serikali kwa ujumla.


Post a Comment

Mpya zaidi Nzee zaidi